36:28Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
36:29Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
36:30Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
36:31Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
36:32Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
36:33Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
36:34Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
36:35Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
36:36Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
36:37Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
36:38Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
36:39Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
36:40Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.