78:1WANAULIZANA nini?
78:2Ile khabari kuu,
78:3Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
78:4La! Karibu watakuja jua.
78:5Tena la! Karibu watakuja jua.
78:6Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
78:7Na milima kama vigingi?
78:8Na tukakuumbeni kwa jozi?
78:9Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
78:10Na tukaufanya usiku ni nguo?
78:11Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
78:12Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
78:13Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
78:14Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
78:15Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
78:16Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
78:17Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
78:18Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
78:19Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
78:20Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
78:21Hakika Jahannamu inangojea!
78:22Kwa walio asi ndio makaazi yao,
78:23Wakae humo karne baada ya karne,
78:24Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
78:25Ila maji yamoto sana na usaha,
78:26Ndio jaza muwafaka.
78:27Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
78:28Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
78:29Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
78:30Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!