23:1HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
23:2Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
23:3Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
23:4Na ambao wanatoa Zaka,
23:5Na ambao wanazilinda tupu zao,
23:6Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
23:7Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
23:8Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
23:9Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
23:10Hao ndio warithi,
23:11Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
23:12Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
23:13Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
23:14Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
23:15Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
23:16Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
23:17Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.