37:1Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
37:2Na kwa wenye kukataza mabaya.
37:3Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
37:4Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
37:5Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
37:6Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
37:7Na kulinda na kila shet'ani a'si.
37:8Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
37:9Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
37:10Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
37:11Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
37:12Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
37:13Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
37:14Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
37:15Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
37:16Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
37:17Hata baba zetu wa zamani?
37:18Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
37:19Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
37:20Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
37:21Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
37:22Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
37:23Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
37:24Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa: