38:1S'ad, Naapa kwa Qur'ani yenye mawaidha.
38:2Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani
38:3Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.
38:4Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
38:5Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.
38:6Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa.
38:7Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.
38:8Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu.
38:9Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?
38:10Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!
38:11Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa.
38:12Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo.
38:13Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi.
38:14Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu.
38:15Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.
38:16Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu.