50:1Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
50:2Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
50:3Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
50:4Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
50:5Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
50:6Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
50:7Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
50:8Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
50:9Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
50:10Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
50:11Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
50:12Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
50:13Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
50:14Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
50:15Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.