53:45Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
53:46Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
53:47Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
53:48Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
53:49Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
53:50Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
53:51Na Thamudi hakuwabakisha,
53:52Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
53:53Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
53:54Vikaifunika vilivyo funika.
53:55Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
53:56Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
53:57Kiyama kimekaribia!
53:58Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
53:59Je! Mnayastaajabia maneno haya?
53:60Na mnacheka, wala hamlii?
53:61Nanyi mmeghafilika?
53:62Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
54:1Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
54:2Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
54:3Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
54:4Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
54:5Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
54:6Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;