73:1Ewe uliye jifunika!
73:2Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!
73:3Nusu yake, au ipunguze kidogo.
73:4Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
73:5Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.
73:6Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
73:7Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.
73:8Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
73:9Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
73:10Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
73:11Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
73:12Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
73:13Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
73:14Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!
73:15Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
73:16Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
73:17Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
73:18Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
73:19Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.