74:48Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
74:49Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
74:50Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
74:51Wanao mkimbia simba!
74:52Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
74:53Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
74:54Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
74:55Basi anaye taka atakumbuka.
74:56Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
75:1Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
75:2Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
75:3Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
75:4Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
75:5Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
75:6Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
75:7Basi jicho litapo dawaa,
75:8Na mwezi utapo patwa,
75:9Na likakusanywa jua na mwezi,
75:10Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
75:11La! Hapana pa kukimbilia!
75:12Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
75:13Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
75:14Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
75:15Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
75:16Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
75:17Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
75:18Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
75:19Kisha ni juu yetu kuubainisha.