78:31Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
78:32Mabustani na mizabibu,
78:33Na wake walio lingana nao,
78:34Na bilauri zilizo jaa,
78:35Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
78:36Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
78:37Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
78:38Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
78:39Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
78:40Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
79:1Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
79:2Na kwa wanao toa kwa upole,
79:3Na wanao ogelea,
79:4Wakishindana mbio,
79:5Wakidabiri mambo.
79:6Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
79:7Kifuate cha kufuatia.
79:8Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
79:9Macho yatainama chini.
79:10Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
79:11Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
79:12Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
79:13Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
79:14Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
79:15Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
79:16Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia: