80:1Alikunja kipaji na akageuka,
80:2Kwa sababu alimjia kipofu!
80:3Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
80:4Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
80:5Ama ajionaye hana haja,
80:6Wewe ndio unamshughulikia?
80:7Na si juu yako kama hakutakasika.
80:8Ama anaye kujia kwa juhudi,
80:9Naye anaogopa,
80:10Ndio wewe unampuuza?
80:11Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
80:12Basi anaye penda akumbuke.
80:13Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
80:14Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
80:15Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
80:16Watukufu, wema.
80:17Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
80:18Kwa kitu gani amemuumba?
80:19Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
80:20Kisha akamsahilishia njia.
80:21Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
80:22Kisha apendapo atamfufua.
80:23La! Hajamaliza aliyo muamuru.
80:24Hebu mtu na atazame chakula chake.
80:25Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
80:26Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
80:27Kisha tukaotesha humo nafaka,
80:28Na zabibu, na mimea ya majani,
80:29Na mizaituni, na mitende,
80:30Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
80:31Na matunda, na malisho ya wanyama;
80:32Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
80:33Basi utakapo kuja ukelele,
80:34Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
80:35Na mamaye na babaye,
80:36Na mkewe na wanawe -
80:37Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
80:38Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
80:39Zitacheka, zitachangamka;
80:40Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,