86:1Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
86:2Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
86:3Ni Nyota yenye mwanga mkali.
86:4Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
86:5Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
86:6Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
86:7Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
86:8Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
86:9Siku zitakapo dhihirishwa siri.
86:10Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
86:11Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
86:12Na kwa ardhi inayo pasuka!
86:13Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
86:14Wala si mzaha.
86:15Hakika wao wanapanga mpango.
86:16Na Mimi napanga mpango.
86:17Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
87:1Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
87:2Aliye umba, na akaweka sawa,
87:3Na ambaye amekadiria na akaongoa,
87:4Na aliye otesha malisho,
87:5Kisha akayafanya makavu, meusi.
87:6Tutakusomesha wala hutasahau,
87:7Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
87:8Na tutakusahilishia yawe mepesi.
87:9Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
87:10Atakumbuka mwenye kuogopa.