87:11Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
87:12Ambaye atauingia Moto mkubwa.
87:13Tena humo hatakufa wala hawi hai.
87:14Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
87:15Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
87:16Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
87:17Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
87:18Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
87:19Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
88:1Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
88:2Siku hiyo nyuso zitainama,
88:3Zikifanya kazi, nazo taabani.
88:4Ziingie katika Moto unao waka -
88:5Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
88:6Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
88:7Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
88:8Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
88:9Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
88:10Katika Bustani ya juu.
88:11Hawatasikia humo upuuzi.
88:12Humo imo chemchem inayo miminika.
88:13Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
88:14Na bilauri zilizo pangwa,
88:15Na matakia safu safu,
88:16Na mazulia yaliyo tandikwa.
88:17Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
88:18Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
88:19Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
88:20Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
88:21Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
88:22Wewe si mwenye kuwatawalia.