88:23Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
88:24Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
88:25Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
88:26Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
89:1Naapa kwa alfajiri,
89:2Na kwa masiku kumi,
89:3Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
89:4Na kwa usiku unapo pita,
89:5Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
89:6Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
89:7Wa Iram, wenye majumba marefu?
89:8Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
89:9Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
89:10Na Firauni mwenye vigingi?
89:11Ambao walifanya jeuri katika nchi?
89:12Wakakithirisha humo ufisadi?
89:13Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
89:14Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
89:15Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
89:16Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
89:17Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
89:18Wala hamhimizani kulisha masikini;
89:19Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
89:20Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
89:21Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
89:22Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,