92:10Tutamsahilishia yawe mazito!
92:11Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
92:12Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
92:13Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
92:14Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
92:15Hatauingia ila mwovu kabisa!
92:16Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
92:17Na mchamngu ataepushwa nao,
92:18Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
92:19Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
92:20Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
92:21Naye atakuja ridhika!
93:1Naapa kwa mchana!
93:2Na kwa usiku unapo tanda!
93:3Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
93:4Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
93:5Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
93:6Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
93:7Na akakukuta umepotea akakuongoa?
93:8Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
93:9Basi yatima usimwonee!
93:10Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
93:11Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
94:1Hatukukunjulia kifua chako?
94:2Na tukakuondolea mzigo wako,