إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِنْ أَهْلِ ٱلْكِتَـٰبِ وَٱلْمُشْرِكِينَ فِى نَارِ جَهَنَّمَ خَـٰلِدِينَ فِيهَآ ۚ أُو۟لَـٰٓئِكَ هُمْ شَرُّ ٱلْبَرِيَّةِ﴿٦﴾إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ أُو۟لَـٰٓئِكَ هُمْ خَيْرُ ٱلْبَرِيَّةِ﴿٧﴾جَزَآؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّـٰتُ عَدْنٍ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَـٰرُ خَـٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًا ۖ رَّضِىَ ٱللَّهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا۟ عَنْهُ ۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِىَ رَبَّهُۥ﴿٨﴾
98:6Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa.
98:7Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe.
98:8Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yu radhi nao, na wao waradhi naye. Hayo ni kwa anaye mwogopa Mola wake Mlezi.
الزلزلةAz-Zalzalahبِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
إِذَا زُلْزِلَتِ ٱلْأَرْضُ زِلْزَالَهَا﴿١﴾وَأَخْرَجَتِ ٱلْأَرْضُ أَثْقَالَهَا﴿٢﴾وَقَالَ ٱلْإِنسَـٰنُ مَا لَهَا﴿٣﴾يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا﴿٤﴾بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا﴿٥﴾يَوْمَئِذٍ يَصْدُرُ ٱلنَّاسُ أَشْتَاتًا لِّيُرَوْا۟ أَعْمَـٰلَهُمْ﴿٦﴾فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُۥ﴿٧﴾وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُۥ﴿٨﴾
99:1Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
99:2Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
99:3Na mtu akasema: Ina nini?
99:4Siku hiyo itahadithia khabari zake.
99:5Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
99:6Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
99:7Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
99:8Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
العادياتAl-'Adiyatبِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
وَٱلْعَـٰدِيَـٰتِ ضَبْحًا﴿١﴾فَٱلْمُورِيَـٰتِ قَدْحًا﴿٢﴾فَٱلْمُغِيرَٰتِ صُبْحًا﴿٣﴾فَأَثَرْنَ بِهِۦ نَقْعًا﴿٤﴾فَوَسَطْنَ بِهِۦ جَمْعًا﴿٥﴾
100:1Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
100:2Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
100:3Wakishambulia wakati wa asubuhi,
100:4Huku wakitimua vumbi,
100:5Na wakijitoma kati ya kundi,