Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/99

الحجر

Al-Hijr

Hicr

Makkiyya·Aya 99

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

15:1
Juz 14
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

الٓر ۚ تِلْكَ ءَايَـٰتُ ٱلْكِتَـٰبِ وَقُرْءَانٍ مُّبِينٍ﴿١﴾

Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.

—
15:2
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَوْ كَانُوا۟ مُسْلِمِينَ﴿٢﴾

HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.

—
15:3
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا۟ وَيَتَمَتَّعُوا۟ وَيُلْهِهِمُ ٱلْأَمَلُ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ﴿٣﴾

Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.

—
15:4
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٌ مَّعْلُومٌ﴿٤﴾

Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.

—
15:5
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

مَّا تَسْبِقُ مِنْ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسْتَـْٔخِرُونَ﴿٥﴾

Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.

—
15:6
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

وَقَالُوا۟ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِى نُزِّلَ عَلَيْهِ ٱلذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ﴿٦﴾

Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.

—
15:7
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

لَّوْ مَا تَأْتِينَا بِٱلْمَلَـٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ﴿٧﴾

Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?

—
15:8
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

مَا نُنَزِّلُ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَمَا كَانُوٓا۟ إِذًا مُّنظَرِينَ﴿٨﴾

Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.

—
15:9
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا ٱلذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَـٰفِظُونَ﴿٩﴾

Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.

—
15:10
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ فِى شِيَعِ ٱلْأَوَّلِينَ﴿١٠﴾

Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.

—
15:11
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

وَمَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ﴿١١﴾

Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.

—
15:12
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

كَذَٰلِكَ نَسْلُكُهُۥ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ﴿١٢﴾

Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.

—
15:13
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ ۖ وَقَدْ خَلَتْ سُنَّةُ ٱلْأَوَّلِينَ﴿١٣﴾

Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.

—
15:14
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

وَلَوْ فَتَحْنَا عَلَيْهِم بَابًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّوا۟ فِيهِ يَعْرُجُونَ﴿١٤﴾

Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,

—
15:15
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 262

لَقَالُوٓا۟ إِنَّمَا سُكِّرَتْ أَبْصَـٰرُنَا بَلْ نَحْنُ قَوْمٌ مَّسْحُورُونَ﴿١٥﴾

Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.

—
15:16
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَلَقَدْ جَعَلْنَا فِى ٱلسَّمَآءِ بُرُوجًا وَزَيَّنَّـٰهَا لِلنَّـٰظِرِينَ﴿١٦﴾

Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.

—
15:17
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَحَفِظْنَـٰهَا مِن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ رَّجِيمٍ﴿١٧﴾

Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.

—
15:18
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

إِلَّا مَنِ ٱسْتَرَقَ ٱلسَّمْعَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ مُّبِينٌ﴿١٨﴾

Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.

—
15:19
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَٱلْأَرْضَ مَدَدْنَـٰهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَٰسِىَ وَأَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَىْءٍ مَّوْزُونٍ﴿١٩﴾

Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.

—
15:20
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَجَعَلْنَا لَكُمْ فِيهَا مَعَـٰيِشَ وَمَن لَّسْتُمْ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ﴿٢٠﴾

Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.

—
15:21
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَإِن مِّن شَىْءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٍ مَّعْلُومٍ﴿٢١﴾

Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.

—
15:22
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَأَرْسَلْنَا ٱلرِّيَـٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً فَأَسْقَيْنَـٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمْ لَهُۥ بِخَـٰزِنِينَ﴿٢٢﴾

Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.

—
15:23
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْىِۦ وَنُمِيتُ وَنَحْنُ ٱلْوَٰرِثُونَ﴿٢٣﴾

Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.

—
15:24
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَلَقَدْ عَلِمْنَا ٱلْمُسْتَقْدِمِينَ مِنكُمْ وَلَقَدْ عَلِمْنَا ٱلْمُسْتَـْٔخِرِينَ﴿٢٤﴾

Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.

—
15:25
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحْشُرُهُمْ ۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٌ﴿٢٥﴾

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.

—
15:26
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَلَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ مِن صَلْصَـٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ﴿٢٦﴾

Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

—
15:27
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَٱلْجَآنَّ خَلَقْنَـٰهُ مِن قَبْلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ﴿٢٧﴾

Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.

—
15:28
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّى خَـٰلِقٌۢ بَشَرًا مِّن صَلْصَـٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ﴿٢٨﴾

Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

—
15:29
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

فَإِذَا سَوَّيْتُهُۥ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِى فَقَعُوا۟ لَهُۥ سَـٰجِدِينَ﴿٢٩﴾

Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.

—
15:30
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

فَسَجَدَ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ﴿٣٠﴾

Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,

—
15:31
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 263

إِلَّآ إِبْلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ﴿٣١﴾

Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.

—
15:32
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ يَـٰٓإِبْلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ﴿٣٢﴾

(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?

—
15:33
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ لَمْ أَكُن لِّأَسْجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقْتَهُۥ مِن صَلْصَـٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ﴿٣٣﴾

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.

—
15:34
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ فَٱخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ﴿٣٤﴾

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!

—
15:35
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

وَإِنَّ عَلَيْكَ ٱللَّعْنَةَ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلدِّينِ﴿٣٥﴾

Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

—
15:36
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِىٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ﴿٣٦﴾

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.

—
15:37
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلْمُنظَرِينَ﴿٣٧﴾

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula

—
15:38
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْوَقْتِ ٱلْمَعْلُومِ﴿٣٨﴾

Mpaka siku ya wakati maalumu.

—
15:39
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغْوَيْتَنِى لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمْ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ﴿٣٩﴾

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,

—
15:40
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ ٱلْمُخْلَصِينَ﴿٤٠﴾

Ila waja wako walio safika.

—
15:41
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

قَالَ هَـٰذَا صِرَٰطٌ عَلَىَّ مُسْتَقِيمٌ﴿٤١﴾

Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.

—
15:42
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

إِنَّ عِبَادِى لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَـٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْغَاوِينَ﴿٤٢﴾

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.

—
15:43
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوْعِدُهُمْ أَجْمَعِينَ﴿٤٣﴾

Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.

—
15:44
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

لَهَا سَبْعَةُ أَبْوَٰبٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنْهُمْ جُزْءٌ مَّقْسُومٌ﴿٤٤﴾

Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.

—
15:45
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ﴿٤٥﴾

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

—
15:46
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

ٱدْخُلُوهَا بِسَلَـٰمٍ ءَامِنِينَ﴿٤٦﴾

(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.

—
15:47
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

وَنَزَعْنَا مَا فِى صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ إِخْوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ﴿٤٧﴾

Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.

—
15:48
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ﴿٤٨﴾

Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.

—
15:49
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

۞ نَبِّئْ عِبَادِىٓ أَنِّىٓ أَنَا ٱلْغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ﴿٤٩﴾

Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.

—
15:50
Juz 14 · Hizb 27 · Ukurasa 264

وَأَنَّ عَذَابِى هُوَ ٱلْعَذَابُ ٱلْأَلِيمُ﴿٥٠﴾

Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!

—
Aya IliyotanguliaIbrahimAya InayofuataAn-Nahl