15:1Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
15:2HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
15:3Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
15:4Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
15:5Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
15:6Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
15:7Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
15:8Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
15:9Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
15:10Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
15:11Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
15:12Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
15:13Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
15:14Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
15:15Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.