Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/227

الشعراء

Ash-Shu'ara

Şuarâ

Makkiyya·Aya 227

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

26:1
Juz 19
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

طسٓمٓ﴿١﴾

T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)

—
26:2
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

تِلْكَ ءَايَـٰتُ ٱلْكِتَـٰبِ ٱلْمُبِينِ﴿٢﴾

Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

—
26:3
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

لَعَلَّكَ بَـٰخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ﴿٣﴾

Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

—
26:4
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةً فَظَلَّتْ أَعْنَـٰقُهُمْ لَهَا خَـٰضِعِينَ﴿٤﴾

Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.

—
26:5
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ ٱلرَّحْمَـٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ﴿٥﴾

Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.

—
26:6
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَـٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ﴿٦﴾

Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.

—
26:7
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ﴿٧﴾

Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

—
26:8
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ﴿٨﴾

Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

—
26:9
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ﴿٩﴾

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

—
26:10
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ﴿١٠﴾

Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,

—
26:11
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ﴿١١﴾

Watu wa Firauni. Hawaogopi?

—
26:12
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ﴿١٢﴾

Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.

—
26:13
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَـٰرُونَ﴿١٣﴾

Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

—
26:14
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ﴿١٤﴾

Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.

—
26:15
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

قَالَ كَلَّا ۖ فَٱذْهَبَا بِـَٔايَـٰتِنَآ ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ﴿١٥﴾

Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

—
26:16
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ﴿١٦﴾

Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

—
26:17
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ﴿١٧﴾

Waachilie Wana wa Israili wende nasi.

—
26:18
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ﴿١٨﴾

(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?

—
26:19
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 367

وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَـٰفِرِينَ﴿١٩﴾

Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?

—
26:20
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ﴿٢٠﴾

(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.

—
26:21
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ﴿٢١﴾

Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

—
26:22
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ﴿٢٢﴾

Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

—
26:23
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَـٰلَمِينَ﴿٢٣﴾

Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

—
26:24
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ﴿٢٤﴾

Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

—
26:25
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ﴿٢٥﴾

(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?

—
26:26
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ﴿٢٦﴾

(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

—
26:27
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ﴿٢٧﴾

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.

—
26:28
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ﴿٢٨﴾

(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

—
26:29
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَـٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ﴿٢٩﴾

(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

—
26:30
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍ مُّبِينٍ﴿٣٠﴾

Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

—
26:31
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ﴿٣١﴾

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.

—
26:32
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ﴿٣٢﴾

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.

—
26:33
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ﴿٣٣﴾

Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.

—
26:34
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَـٰذَا لَسَـٰحِرٌ عَلِيمٌ﴿٣٤﴾

(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

—
26:35
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ﴿٣٥﴾

Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

—
26:36
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَـٰشِرِينَ﴿٣٦﴾

Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.

—
26:37
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ﴿٣٧﴾

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

—
26:38
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ﴿٣٨﴾

Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.

—
26:39
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 368

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ﴿٣٩﴾

Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?

—
26:40
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَـٰلِبِينَ﴿٤٠﴾

Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.

—
26:41
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَـٰلِبِينَ﴿٤١﴾

Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?

—
26:42
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ﴿٤٢﴾

Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

—
26:43
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ﴿٤٣﴾

Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.

—
26:44
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَـٰلِبُونَ﴿٤٤﴾

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

—
26:45
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ﴿٤٥﴾

Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.

—
26:46
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَـٰجِدِينَ﴿٤٦﴾

Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.

—
26:47
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ﴿٤٧﴾

Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

—
26:48
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَـٰرُونَ﴿٤٨﴾

Mola Mlezi wa Musa na Harun.

—
26:49
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَـٰفٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ﴿٤٩﴾

(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.

—
26:50
Juz 19 · Hizb 37 · Ukurasa 369

قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ﴿٥٠﴾

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

—
Aya IliyotanguliaAl-FurqanAya InayofuataAn-Naml