26:1T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
26:2Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
26:3Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
26:4Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
26:5Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
26:6Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
26:7Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
26:8Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
26:9Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
26:10Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
26:11Watu wa Firauni. Hawaogopi?
26:12Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
26:13Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
26:14Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
26:15Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
26:16Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
26:17Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
26:18(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
26:19Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?