Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/59

الدخان

Ad-Dukhan

Duhân

Makkiyya·Aya 59

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

44:1
Juz 25
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

حمٓ﴿١﴾

H'a Mim

—
44:2
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

وَٱلْكِتَـٰبِ ٱلْمُبِينِ﴿٢﴾

Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,

—
44:3
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

إِنَّآ أَنزَلْنَـٰهُ فِى لَيْلَةٍ مُّبَـٰرَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ﴿٣﴾

Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.

—
44:4
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ﴿٤﴾

Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,

—
44:5
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

أَمْرًا مِّنْ عِندِنَآ ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ﴿٥﴾

Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.

—
44:6
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ﴿٦﴾

Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.

—
44:7
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

رَبِّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ﴿٧﴾

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.

—
44:8
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْىِۦ وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ﴿٨﴾

Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.

—
44:9
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

بَلْ هُمْ فِى شَكٍّ يَلْعَبُونَ﴿٩﴾

Lakini wao wanacheza katika shaka.

—
44:10
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

فَٱرْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِى ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ﴿١٠﴾

Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,

—
44:11
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

يَغْشَى ٱلنَّاسَ ۖ هَـٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿١١﴾

Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!

—
44:12
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

رَّبَّنَا ٱكْشِفْ عَنَّا ٱلْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ﴿١٢﴾

Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.

—
44:13
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَآءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ﴿١٣﴾

Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.

—
44:14
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

ثُمَّ تَوَلَّوْا۟ عَنْهُ وَقَالُوا۟ مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ﴿١٤﴾

Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.

—
44:15
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

إِنَّا كَاشِفُوا۟ ٱلْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَآئِدُونَ﴿١٥﴾

Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!

—
44:16
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

يَوْمَ نَبْطِشُ ٱلْبَطْشَةَ ٱلْكُبْرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ﴿١٦﴾

Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.

—
44:17
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

۞ وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَآءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ﴿١٧﴾

Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.

—
44:18
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 496

أَنْ أَدُّوٓا۟ إِلَىَّ عِبَادَ ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ﴿١٨﴾

Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.

—
44:19
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَأَن لَّا تَعْلُوا۟ عَلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّىٓ ءَاتِيكُم بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ﴿١٩﴾

Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.

—
44:20
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَإِنِّى عُذْتُ بِرَبِّى وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ﴿٢٠﴾

Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.

—
44:21
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا۟ لِى فَٱعْتَزِلُونِ﴿٢١﴾

Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.

—
44:22
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ﴿٢٢﴾

Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.

—
44:23
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

فَأَسْرِ بِعِبَادِى لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ﴿٢٣﴾

Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.

—
44:24
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَٱتْرُكِ ٱلْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ﴿٢٤﴾

Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.

—
44:25
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

كَمْ تَرَكُوا۟ مِن جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ﴿٢٥﴾

Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!

—
44:26
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ﴿٢٦﴾

Na mimea na vyeo vitukufu!

—
44:27
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَنَعْمَةٍ كَانُوا۟ فِيهَا فَـٰكِهِينَ﴿٢٧﴾

Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!

—
44:28
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَـٰهَا قَوْمًا ءَاخَرِينَ﴿٢٨﴾

Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.

—
44:29
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلْأَرْضُ وَمَا كَانُوا۟ مُنظَرِينَ﴿٢٩﴾

La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.

—
44:30
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ مِنَ ٱلْعَذَابِ ٱلْمُهِينِ﴿٣٠﴾

Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,

—
44:31
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيًا مِّنَ ٱلْمُسْرِفِينَ﴿٣١﴾

Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.

—
44:32
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَلَقَدِ ٱخْتَرْنَـٰهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى ٱلْعَـٰلَمِينَ﴿٣٢﴾

Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.

—
44:33
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَءَاتَيْنَـٰهُم مِّنَ ٱلْـَٔايَـٰتِ مَا فِيهِ بَلَـٰٓؤٌا۟ مُّبِينٌ﴿٣٣﴾

Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.

—
44:34
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ﴿٣٤﴾

Hakika hawa wanasema:

—
44:35
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

إِنْ هِىَ إِلَّا مَوْتَتُنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ﴿٣٥﴾

Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.

—
44:36
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

فَأْتُوا۟ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ﴿٣٦﴾

Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.

—
44:37
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَـٰهُمْ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ مُجْرِمِينَ﴿٣٧﴾

Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.

—
44:38
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

وَمَا خَلَقْنَا ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَـٰعِبِينَ﴿٣٨﴾

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.

—
44:39
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 497

مَا خَلَقْنَـٰهُمَآ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ﴿٣٩﴾

Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.

—
44:40
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ مِيقَـٰتُهُمْ أَجْمَعِينَ﴿٤٠﴾

Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.

—
44:41
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

يَوْمَ لَا يُغْنِى مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْـًٔا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ﴿٤١﴾

Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.

—
44:42
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ﴿٤٢﴾

Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

—
44:43
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ﴿٤٣﴾

Hakika Mti wa Zaqqum,

—
44:44
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

طَعَامُ ٱلْأَثِيمِ﴿٤٤﴾

Ni chakula cha mwenye dhambi.

—
44:45
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

كَٱلْمُهْلِ يَغْلِى فِى ٱلْبُطُونِ﴿٤٥﴾

Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni

—
44:46
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

كَغَلْىِ ٱلْحَمِيمِ﴿٤٦﴾

Kama kutokota kwa maji ya moto.

—
44:47
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

خُذُوهُ فَٱعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ﴿٤٧﴾

(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!

—
44:48
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

ثُمَّ صُبُّوا۟ فَوْقَ رَأْسِهِۦ مِنْ عَذَابِ ٱلْحَمِيمِ﴿٤٨﴾

Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.

—
44:49
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ ٱلْعَزِيزُ ٱلْكَرِيمُ﴿٤٩﴾

Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!

—
44:50
Juz 25 · Hizb 50 · Ukurasa 498

إِنَّ هَـٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمْتَرُونَ﴿٥٠﴾

Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.

—
Aya IliyotanguliaAz-ZukhrufAya InayofuataAl-Jathiyah