44:1H'a Mim
44:2Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
44:3Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
44:4Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
44:5Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
44:6Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
44:7Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
44:8Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
44:9Lakini wao wanacheza katika shaka.
44:10Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
44:11Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
44:12Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
44:13Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
44:14Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
44:15Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
44:16Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
44:17Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
44:18Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.