Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/96

الواقعة

Al-Waqi'ah

Vâkıa

Makkiyya·Aya 96

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

56:1
Juz 27
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ﴿١﴾

Litakapo tukia hilo Tukio

—
56:2
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ﴿٢﴾

Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

—
56:3
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ﴿٣﴾

Literemshalo linyanyualo,

—
56:4
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّا﴿٤﴾

Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

—
56:5
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّا﴿٥﴾

Na milima itapo sagwasagwa,

—
56:6
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

فَكَانَتْ هَبَآءً مُّنۢبَثًّا﴿٦﴾

Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

—
56:7
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًا ثَلَـٰثَةً﴿٧﴾

Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

—
56:8
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

فَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ﴿٨﴾

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

—
56:9
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

وَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ﴿٩﴾

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

—
56:10
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ﴿١٠﴾

Na wa mbele watakuwa mbele.

—
56:11
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

أُو۟لَـٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ﴿١١﴾

Hao ndio watakao karibishwa

—
56:12
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ﴿١٢﴾

Katika Bustani zenye neema.

—
56:13
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ﴿١٣﴾

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

—
56:14
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

وَقَلِيلٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ﴿١٤﴾

Na wachache katika wa mwisho.

—
56:15
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ﴿١٥﴾

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

—
56:16
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 534

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَـٰبِلِينَ﴿١٦﴾

Wakiviegemea wakielekeana.

—
56:17
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ﴿١٧﴾

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

—
56:18
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ﴿١٨﴾

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

—
56:19
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ﴿١٩﴾

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

—
56:20
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَفَـٰكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ﴿٢٠﴾

Na matunda wayapendayo,

—
56:21
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ﴿٢١﴾

Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

—
56:22
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَحُورٌ عِينٌ﴿٢٢﴾

Na Mahurulaini,

—
56:23
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

كَأَمْثَـٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ﴿٢٣﴾

Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

—
56:24
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

جَزَآءًۢ بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ﴿٢٤﴾

Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

—
56:25
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا﴿٢٥﴾

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

—
56:26
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

إِلَّا قِيلًا سَلَـٰمًا سَلَـٰمًا﴿٢٦﴾

Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

—
56:27
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَأَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ﴿٢٧﴾

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

—
56:28
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

فِى سِدْرٍ مَّخْضُودٍ﴿٢٨﴾

Katika mikunazi isiyo na miba,

—
56:29
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ﴿٢٩﴾

Na migomba iliyo pangiliwa,

—
56:30
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ﴿٣٠﴾

Na kivuli kilicho tanda,

—
56:31
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَمَآءٍ مَّسْكُوبٍ﴿٣١﴾

Na maji yanayo miminika,

—
56:32
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَفَـٰكِهَةٍ كَثِيرَةٍ﴿٣٢﴾

Na matunda mengi,

—
56:33
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ﴿٣٣﴾

Hayatindikii wala hayakatazwi,

—
56:34
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ﴿٣٤﴾

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

—
56:35
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

إِنَّآ أَنشَأْنَـٰهُنَّ إِنشَآءً﴿٣٥﴾

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

—
56:36
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

فَجَعَلْنَـٰهُنَّ أَبْكَارًا﴿٣٦﴾

Na tutawafanya vijana,

—
56:37
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

عُرُبًا أَتْرَابًا﴿٣٧﴾

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

—
56:38
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

لِّأَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ﴿٣٨﴾

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

—
56:39
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ﴿٣٩﴾

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

—
56:40
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ﴿٤٠﴾

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

—
56:41
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَأَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ﴿٤١﴾

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

—
56:42
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

فِى سَمُومٍ وَحَمِيمٍ﴿٤٢﴾

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

—
56:43
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ﴿٤٣﴾

Na kivuli cha moshi mweusi,

—
56:44
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ﴿٤٤﴾

Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

—
56:45
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ﴿٤٥﴾

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

—
56:46
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَكَانُوا۟ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ﴿٤٦﴾

Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

—
56:47
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

وَكَانُوا۟ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ﴿٤٧﴾

Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

—
56:48
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ﴿٤٨﴾

Au baba zetu wa zamani?

—
56:49
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْـَٔاخِرِينَ﴿٤٩﴾

Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

—
56:50
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 535

لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ﴿٥٠﴾

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

—
Aya IliyotanguliaAr-RahmanAya InayofuataAl-Hadid