55:70Humo wamo wanawake wema wazuri.
55:71Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
55:72Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
55:73Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
55:74Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
55:75Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
55:76Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
55:77Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
55:78Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
56:1Litakapo tukia hilo Tukio
56:2Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
56:3Literemshalo linyanyualo,
56:4Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
56:5Na milima itapo sagwasagwa,
56:6Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
56:7Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
56:8Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
56:9Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
56:10Na wa mbele watakuwa mbele.
56:11Hao ndio watakao karibishwa
56:12Katika Bustani zenye neema.
56:13Fungu kubwa katika wa mwanzo,
56:14Na wachache katika wa mwisho.
56:15Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
56:16Wakiviegemea wakielekeana.