Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/52

القلم

Al-Qalam

Kalem

Makkiyya·Aya 52

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

68:1
Juz 29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

نٓ ۚ وَٱلْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ﴿١﴾

Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,

—
68:2
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

مَآ أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ﴿٢﴾

Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

—
68:3
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ﴿٣﴾

Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.

—
68:4
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤﴾

Na hakika wewe una tabia tukufu.

—
68:5
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ﴿٥﴾

Karibu utaona, na wao wataona,

—
68:6
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

بِأَييِّكُمُ ٱلْمَفْتُونُ﴿٦﴾

Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.

—
68:7
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِٱلْمُهْتَدِينَ﴿٧﴾

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.

—
68:8
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

فَلَا تُطِعِ ٱلْمُكَذِّبِينَ﴿٨﴾

Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.

—
68:9
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

وَدُّوا۟ لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ﴿٩﴾

Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.

—
68:10
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ﴿١٠﴾

Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,

—
68:11
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

هَمَّازٍ مَّشَّآءٍۭ بِنَمِيمٍ﴿١١﴾

Mtapitapi, apitaye akifitini,

—
68:12
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ﴿١٢﴾

Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,

—
68:13
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

عُتُلٍّۭ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ﴿١٣﴾

Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.

—
68:14
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ﴿١٤﴾

Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

—
68:15
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَـٰتُنَا قَالَ أَسَـٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ﴿١٥﴾

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!

—
68:16
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 564

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلْخُرْطُومِ﴿١٦﴾

Tutamtia kovu juu ya pua yake.

—
68:17
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

إِنَّا بَلَوْنَـٰهُمْ كَمَا بَلَوْنَآ أَصْحَـٰبَ ٱلْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا۟ لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ﴿١٧﴾

Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.

—
68:18
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

وَلَا يَسْتَثْنُونَ﴿١٨﴾

Wala hawakusema: Mungu akipenda!

—
68:19
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

فَطَافَ عَلَيْهَا طَآئِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَآئِمُونَ﴿١٩﴾

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

—
68:20
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

فَأَصْبَحَتْ كَٱلصَّرِيمِ﴿٢٠﴾

Likawa kama usiku wa giza.

—
68:21
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

فَتَنَادَوْا۟ مُصْبِحِينَ﴿٢١﴾

Asubuhi wakaitana.

—
68:22
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

أَنِ ٱغْدُوا۟ عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰرِمِينَ﴿٢٢﴾

Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

—
68:23
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

فَٱنطَلَقُوا۟ وَهُمْ يَتَخَـٰفَتُونَ﴿٢٣﴾

Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,

—
68:24
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا ٱلْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ﴿٢٤﴾

Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.

—
68:25
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

وَغَدَوْا۟ عَلَىٰ حَرْدٍ قَـٰدِرِينَ﴿٢٥﴾

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

—
68:26
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوٓا۟ إِنَّا لَضَآلُّونَ﴿٢٦﴾

Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!

—
68:27
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ﴿٢٧﴾

Bali tumenyimwa!

—
68:28
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ﴿٢٨﴾

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

—
68:29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

قَالُوا۟ سُبْحَـٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَـٰلِمِينَ﴿٢٩﴾

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

—
68:30
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَـٰوَمُونَ﴿٣٠﴾

Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

—
68:31
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

قَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَـٰغِينَ﴿٣١﴾

Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

—
68:32
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ﴿٣٢﴾

Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

—
68:33
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

كَذَٰلِكَ ٱلْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ ٱلْـَٔاخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا۟ يَعْلَمُونَ﴿٣٣﴾

Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!

—
68:34
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ﴿٣٤﴾

Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

—
68:35
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

أَفَنَجْعَلُ ٱلْمُسْلِمِينَ كَٱلْمُجْرِمِينَ﴿٣٥﴾

Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

—
68:36
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ﴿٣٦﴾

Mna nini? Mnahukumu vipi?

—
68:37
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

أَمْ لَكُمْ كِتَـٰبٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ﴿٣٧﴾

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

—
68:38
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ﴿٣٨﴾

Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?

—
68:39
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

أَمْ لَكُمْ أَيْمَـٰنٌ عَلَيْنَا بَـٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْقِيَـٰمَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ﴿٣٩﴾

Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?

—
68:40
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ﴿٤٠﴾

Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?

—
68:41
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

أَمْ لَهُمْ شُرَكَآءُ فَلْيَأْتُوا۟ بِشُرَكَآئِهِمْ إِن كَانُوا۟ صَـٰدِقِينَ﴿٤١﴾

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

—
68:42
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 565

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ﴿٤٢﴾

Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,

—
68:43
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

خَـٰشِعَةً أَبْصَـٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا۟ يُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمْ سَـٰلِمُونَ﴿٤٣﴾

Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -

—
68:44
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

فَذَرْنِى وَمَن يُكَذِّبُ بِهَـٰذَا ٱلْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ﴿٤٤﴾

Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.

—
68:45
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

وَأُمْلِى لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِى مَتِينٌ﴿٤٥﴾

Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

—
68:46
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ﴿٤٦﴾

Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

—
68:47
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ﴿٤٧﴾

Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

—
68:48
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ﴿٤٨﴾

Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.

—
68:49
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

لَّوْلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ﴿٤٩﴾

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

—
68:50
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

فَٱجْتَبَـٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ﴿٥٠﴾

Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

—
Aya IliyotanguliaAl-MulkAya InayofuataAl-Haqqah