67:27Lakini watakapo iona karibu, nyuso za walio kufuru zitahuzunishwa, na itasemwa: Hayo ndiyo mliyo kuwa mkiyaomba.
67:28Sema: Mwaonaje, ikiwa Mwenyezi Mungu atanihiliki mimi na walio pamoja nami, au akiturehemu, ni nani atakaye walinda makafiri na adhabu chungu?
67:29Sema: Yeye ndiye Mwingi wa Rehema; tunamuamini Yeye, na juu yake tunategemea. Mtakuja jua ni nani aliye katika upotovu ulio dhaahiri.
67:30Sema: Mwaonaje, yakiwa maji yenu yamedidimia chini, nani atakueleteeni maji yanayo miminika?
68:1Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
68:2Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
68:3Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
68:4Na hakika wewe una tabia tukufu.
68:5Karibu utaona, na wao wataona,
68:6Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
68:7Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
68:8Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
68:9Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
68:10Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
68:11Mtapitapi, apitaye akifitini,
68:12Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
68:13Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
68:14Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
68:15Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
68:16Tutamtia kovu juu ya pua yake.