Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/31

الإنسان

Al-Insan

İnsân

Madaniyya·Aya 31

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

76:1
Juz 29
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 578

هَلْ أَتَىٰ عَلَى ٱلْإِنسَـٰنِ حِينٌ مِّنَ ٱلدَّهْرِ لَمْ يَكُن شَيْـًٔا مَّذْكُورًا﴿١﴾

Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.

—
76:2
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 578

إِنَّا خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَـٰهُ سَمِيعًۢا بَصِيرًا﴿٢﴾

Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.

—
76:3
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 578

إِنَّا هَدَيْنَـٰهُ ٱلسَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا﴿٣﴾

Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.

—
76:4
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 578

إِنَّآ أَعْتَدْنَا لِلْكَـٰفِرِينَ سَلَـٰسِلَا۟ وَأَغْلَـٰلًا وَسَعِيرًا﴿٤﴾

Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.

—
76:5
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 578

إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا﴿٥﴾

Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,

—
76:6
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا عِبَادُ ٱللَّهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفْجِيرًا﴿٦﴾

Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.

—
76:7
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

يُوفُونَ بِٱلنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُۥ مُسْتَطِيرًا﴿٧﴾

Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,

—
76:8
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَيُطْعِمُونَ ٱلطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا﴿٨﴾

Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.

—
76:9
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ ٱللَّهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَآءً وَلَا شُكُورًا﴿٩﴾

Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.

—
76:10
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوْمًا عَبُوسًا قَمْطَرِيرًا﴿١٠﴾

Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.

—
76:11
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

فَوَقَىٰهُمُ ٱللَّهُ شَرَّ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمِ وَلَقَّىٰهُمْ نَضْرَةً وَسُرُورًا﴿١١﴾

Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.

—
76:12
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُوا۟ جَنَّةً وَحَرِيرًا﴿١٢﴾

Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.

—
76:13
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ ۖ لَا يَرَوْنَ فِيهَا شَمْسًا وَلَا زَمْهَرِيرًا﴿١٣﴾

Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.

—
76:14
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَدَانِيَةً عَلَيْهِمْ ظِلَـٰلُهَا وَذُلِّلَتْ قُطُوفُهَا تَذْلِيلًا﴿١٤﴾

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.

—
76:15
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَيُطَافُ عَلَيْهِم بِـَٔانِيَةٍ مِّن فِضَّةٍ وَأَكْوَابٍ كَانَتْ قَوَارِيرَا۠﴿١٥﴾

Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,

—
76:16
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

قَوَارِيرَا۟ مِن فِضَّةٍ قَدَّرُوهَا تَقْدِيرًا﴿١٦﴾

Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.

—
76:17
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَيُسْقَوْنَ فِيهَا كَأْسًا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا﴿١٧﴾

Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.

—
76:18
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

عَيْنًا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلْسَبِيلًا﴿١٨﴾

Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.

—
76:19
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

۞ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيْتَهُمْ حَسِبْتَهُمْ لُؤْلُؤًا مَّنثُورًا﴿١٩﴾

Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.

—
76:20
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَإِذَا رَأَيْتَ ثَمَّ رَأَيْتَ نَعِيمًا وَمُلْكًا كَبِيرًا﴿٢٠﴾

Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.

—
76:21
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

عَـٰلِيَهُمْ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضْرٌ وَإِسْتَبْرَقٌ ۖ وَحُلُّوٓا۟ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٍ وَسَقَىٰهُمْ رَبُّهُمْ شَرَابًا طَهُورًا﴿٢١﴾

Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.

—
76:22
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

إِنَّ هَـٰذَا كَانَ لَكُمْ جَزَآءً وَكَانَ سَعْيُكُم مَّشْكُورًا﴿٢٢﴾

Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.

—
76:23
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا عَلَيْكَ ٱلْقُرْءَانَ تَنزِيلًا﴿٢٣﴾

Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.

—
76:24
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعْ مِنْهُمْ ءَاثِمًا أَوْ كَفُورًا﴿٢٤﴾

Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.

—
76:25
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 579

وَٱذْكُرِ ٱسْمَ رَبِّكَ بُكْرَةً وَأَصِيلًا﴿٢٥﴾

Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;

—
76:26
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 580

وَمِنَ ٱلَّيْلِ فَٱسْجُدْ لَهُۥ وَسَبِّحْهُ لَيْلًا طَوِيلًا﴿٢٦﴾

Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.

—
76:27
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 580

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ يُحِبُّونَ ٱلْعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَآءَهُمْ يَوْمًا ثَقِيلًا﴿٢٧﴾

Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.

—
76:28
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 580

نَّحْنُ خَلَقْنَـٰهُمْ وَشَدَدْنَآ أَسْرَهُمْ ۖ وَإِذَا شِئْنَا بَدَّلْنَآ أَمْثَـٰلَهُمْ تَبْدِيلًا﴿٢٨﴾

Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.

—
76:29
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 580

إِنَّ هَـٰذِهِۦ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلًا﴿٢٩﴾

Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.

—
76:30
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 580

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿٣٠﴾

Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.

—
76:31
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 580

يُدْخِلُ مَن يَشَآءُ فِى رَحْمَتِهِۦ ۚ وَٱلظَّـٰلِمِينَ أَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًۢا﴿٣١﴾

Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.

—
Aya IliyotanguliaAl-QiyamahAya InayofuataAl-Mursalat