75:20Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
75:21Na mnaacha maisha ya Akhera.
75:22Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
75:23Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
75:24Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
75:25Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
75:26La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
75:27Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
75:28Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
75:29Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
75:30Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
75:31Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
75:32Bali alikanusha, na akageuka.
75:33Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
75:34Ole wako, ole wako!
75:35Kisha Ole wako, ole wako!
75:36Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
75:37Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
75:38Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
75:39Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
75:40Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
76:1Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
76:2Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
76:3Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
76:4Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
76:5Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,