Inapakia...
1:1KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
1:2Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;
1:3Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;
1:4Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.
1:5Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.
1:6Tuongoe njia iliyo nyooka,
1:7Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.