51:31AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
51:32Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
51:33Tuwatupie mawe ya udongo,
51:34Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
51:35Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
51:36Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
51:37Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
51:38Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
51:39Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
51:40Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
51:41Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
51:42Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
51:43Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
51:44Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
51:45Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
51:46Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
51:47Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
51:48Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
51:49Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
51:50Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
51:51Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.