Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/60

الذاريات

Adh-Dhariyat

Zâriyât

Makkiyya·Aya 60

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

51:1
Juz 26
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 520

وَٱلذَّٰرِيَـٰتِ ذَرْوًا﴿١﴾

Naapa kwa pepo zinazo tawanya,

—
51:2
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 520

فَٱلْحَـٰمِلَـٰتِ وِقْرًا﴿٢﴾

Na zinazo beba mizigo,

—
51:3
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 520

فَٱلْجَـٰرِيَـٰتِ يُسْرًا﴿٣﴾

Na zinazo kwenda kwa wepesi.

—
51:4
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 520

فَٱلْمُقَسِّمَـٰتِ أَمْرًا﴿٤﴾

Na zinazo gawanya kwa amri,

—
51:5
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 520

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ﴿٥﴾

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,

—
51:6
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 520

وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٌ﴿٦﴾

Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.

—
51:7
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْحُبُكِ﴿٧﴾

Naapa kwa mbingu zenye njia,

—
51:8
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

إِنَّكُمْ لَفِى قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ﴿٨﴾

Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.

—
51:9
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ﴿٩﴾

Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.

—
51:10
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

قُتِلَ ٱلْخَرَّٰصُونَ﴿١٠﴾

Wazushi wameangamizwa.

—
51:11
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

ٱلَّذِينَ هُمْ فِى غَمْرَةٍ سَاهُونَ﴿١١﴾

Ambao wameghafilika katika ujinga.

—
51:12
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

يَسْـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلدِّينِ﴿١٢﴾

Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?

—
51:13
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

يَوْمَ هُمْ عَلَى ٱلنَّارِ يُفْتَنُونَ﴿١٣﴾

Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.

—
51:14
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

ذُوقُوا۟ فِتْنَتَكُمْ هَـٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تَسْتَعْجِلُونَ﴿١٤﴾

Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.

—
51:15
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَعُيُونٍ﴿١٥﴾

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

—
51:16
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ﴿١٦﴾

Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

—
51:17
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

كَانُوا۟ قَلِيلًا مِّنَ ٱلَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ﴿١٧﴾

Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.

—
51:18
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

وَبِٱلْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ﴿١٨﴾

Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

—
51:19
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

وَفِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ﴿١٩﴾

Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.

—
51:20
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

وَفِى ٱلْأَرْضِ ءَايَـٰتٌ لِّلْمُوقِنِينَ﴿٢٠﴾

Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

—
51:21
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

وَفِىٓ أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ﴿٢١﴾

Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?

—
51:22
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ﴿٢٢﴾

Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.

—
51:23
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَآ أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ﴿٢٣﴾

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

—
51:24
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ ٱلْمُكْرَمِينَ﴿٢٤﴾

Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?

—
51:25
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَـٰمًا ۖ قَالَ سَلَـٰمٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ﴿٢٥﴾

Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.

—
51:26
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ﴿٢٦﴾

Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.

—
51:27
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ﴿٢٧﴾

Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?

—
51:28
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا۟ لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَـٰمٍ عَلِيمٍ﴿٢٨﴾

Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.

—
51:29
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُۥ فِى صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ﴿٢٩﴾

Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!

—
51:30
Juz 26 · Hizb 52 · Ukurasa 521

قَالُوا۟ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْحَكِيمُ ٱلْعَلِيمُ﴿٣٠﴾

Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.

—
51:31
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

۞ قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ﴿٣١﴾

AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?

—
51:32
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ﴿٣٢﴾

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,

—
51:33
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ﴿٣٣﴾

Tuwatupie mawe ya udongo,

—
51:34
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ﴿٣٤﴾

Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.

—
51:35
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ﴿٣٥﴾

Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.

—
51:36
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ ٱلْمُسْلِمِينَ﴿٣٦﴾

Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

—
51:37
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَتَرَكْنَا فِيهَآ ءَايَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ﴿٣٧﴾

Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.

—
51:38
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَفِى مُوسَىٰٓ إِذْ أَرْسَلْنَـٰهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ﴿٣٨﴾

Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.

—
51:39
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِۦ وَقَالَ سَـٰحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ﴿٣٩﴾

Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!

—
51:40
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَأَخَذْنَـٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذْنَـٰهُمْ فِى ٱلْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ﴿٤٠﴾

Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.

—
51:41
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَفِى عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلْعَقِيمَ﴿٤١﴾

Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.

—
51:42
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

مَا تَذَرُ مِن شَىْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَٱلرَّمِيمِ﴿٤٢﴾

Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.

—
51:43
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَفِى ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا۟ حَتَّىٰ حِينٍ﴿٤٣﴾

Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.

—
51:44
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَعَتَوْا۟ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ﴿٤٤﴾

Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.

—
51:45
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَمَا ٱسْتَطَـٰعُوا۟ مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا۟ مُنتَصِرِينَ﴿٤٥﴾

Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

—
51:46
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَوْمًا فَـٰسِقِينَ﴿٤٦﴾

Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

—
51:47
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَٱلسَّمَآءَ بَنَيْنَـٰهَا بِأَيْي۟دٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ﴿٤٧﴾

Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.

—
51:48
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَٱلْأَرْضَ فَرَشْنَـٰهَا فَنِعْمَ ٱلْمَـٰهِدُونَ﴿٤٨﴾

Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

—
51:49
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

وَمِن كُلِّ شَىْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ﴿٤٩﴾

Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

—
51:50
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 522

فَفِرُّوٓا۟ إِلَى ٱللَّهِ ۖ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ﴿٥٠﴾

Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

—
Aya IliyotanguliaQafAya InayofuataAt-Tur