Sâffât
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفًّا﴿١﴾
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
—فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًا﴿٢﴾
Na kwa wenye kukataza mabaya.
—فَٱلتَّـٰلِيَـٰتِ ذِكْرًا﴿٣﴾
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
—إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌ﴿٤﴾
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
—رَّبُّ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَـٰرِقِ﴿٥﴾
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
—إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ﴿٦﴾
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
—وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَـٰنٍ مَّارِدٍ﴿٧﴾
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
—لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ﴿٨﴾
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
—دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ﴿٩﴾
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
—إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ﴿١٠﴾
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
—فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍۭ﴿١١﴾
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
—بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ﴿١٢﴾
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
—وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ﴿١٣﴾
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
—وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةً يَسْتَسْخِرُونَ﴿١٤﴾
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
—وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَـٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ﴿١٥﴾
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
—أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ﴿١٦﴾
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
—أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ﴿١٧﴾
Hata baba zetu wa zamani?
—قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ﴿١٨﴾
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
—فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ﴿١٩﴾
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
—وَقَالُوا۟ يَـٰوَيْلَنَا هَـٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ﴿٢٠﴾
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
—هَـٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ﴿٢١﴾
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
—۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ﴿٢٢﴾
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
—مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ﴿٢٣﴾
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
—وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ﴿٢٤﴾
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
—مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ﴿٢٥﴾
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
—بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ﴿٢٦﴾
Bali hii leo, watasalimu amri.
—وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ﴿٢٧﴾
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
—قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ﴿٢٨﴾
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
—قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ﴿٢٩﴾
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
—وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَـٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَـٰغِينَ﴿٣٠﴾
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
—فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ﴿٣١﴾
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
—فَأَغْوَيْنَـٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَـٰوِينَ﴿٣٢﴾
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
—فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ﴿٣٣﴾
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
—إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ﴿٣٤﴾
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
—إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ﴿٣٥﴾
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
—وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍۭ﴿٣٦﴾
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
—بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ﴿٣٧﴾
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
—إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ﴿٣٨﴾
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
—وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٣٩﴾
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
—إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ﴿٤٠﴾
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
—أُو۟لَـٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ﴿٤١﴾
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
—فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ﴿٤٢﴾
Matunda, nao watahishimiwa.
—فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ﴿٤٣﴾
Katika Bustani za neema.
—عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَـٰبِلِينَ﴿٤٤﴾
Wako juu ya viti wamekabiliana.
—يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍۭ﴿٤٥﴾
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
—بَيْضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّـٰرِبِينَ﴿٤٦﴾
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
—لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ﴿٤٧﴾
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
—وَعِندَهُمْ قَـٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌ﴿٤٨﴾
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
—كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ﴿٤٩﴾
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
—فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ﴿٥٠﴾
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
—