Vâkıa
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
إِذَا وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ﴿١﴾
Litakapo tukia hilo Tukio
—لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ﴿٢﴾
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
—خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ﴿٣﴾
Literemshalo linyanyualo,
—إِذَا رُجَّتِ ٱلْأَرْضُ رَجًّا﴿٤﴾
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
—وَبُسَّتِ ٱلْجِبَالُ بَسًّا﴿٥﴾
Na milima itapo sagwasagwa,
—فَكَانَتْ هَبَآءً مُّنۢبَثًّا﴿٦﴾
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
—وَكُنتُمْ أَزْوَٰجًا ثَلَـٰثَةً﴿٧﴾
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
—فَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ﴿٨﴾
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
—وَأَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ﴿٩﴾
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
—وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ﴿١٠﴾
Na wa mbele watakuwa mbele.
—أُو۟لَـٰٓئِكَ ٱلْمُقَرَّبُونَ﴿١١﴾
Hao ndio watakao karibishwa
—فِى جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ﴿١٢﴾
Katika Bustani zenye neema.
—ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ﴿١٣﴾
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
—وَقَلِيلٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ﴿١٤﴾
Na wachache katika wa mwisho.
—عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ﴿١٥﴾
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
—مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيْهَا مُتَقَـٰبِلِينَ﴿١٦﴾
Wakiviegemea wakielekeana.
—يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَٰنٌ مُّخَلَّدُونَ﴿١٧﴾
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
—بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ﴿١٨﴾
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
—لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ﴿١٩﴾
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
—وَفَـٰكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ﴿٢٠﴾
Na matunda wayapendayo,
—وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ﴿٢١﴾
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
—وَحُورٌ عِينٌ﴿٢٢﴾
Na Mahurulaini,
—كَأَمْثَـٰلِ ٱللُّؤْلُؤِ ٱلْمَكْنُونِ﴿٢٣﴾
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
—جَزَآءًۢ بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ﴿٢٤﴾
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
—لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا﴿٢٥﴾
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
—إِلَّا قِيلًا سَلَـٰمًا سَلَـٰمًا﴿٢٦﴾
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
—وَأَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلْيَمِينِ﴿٢٧﴾
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
—فِى سِدْرٍ مَّخْضُودٍ﴿٢٨﴾
Katika mikunazi isiyo na miba,
—وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ﴿٢٩﴾
Na migomba iliyo pangiliwa,
—وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ﴿٣٠﴾
Na kivuli kilicho tanda,
—وَمَآءٍ مَّسْكُوبٍ﴿٣١﴾
Na maji yanayo miminika,
—وَفَـٰكِهَةٍ كَثِيرَةٍ﴿٣٢﴾
Na matunda mengi,
—لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ﴿٣٣﴾
Hayatindikii wala hayakatazwi,
—وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ﴿٣٤﴾
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
—إِنَّآ أَنشَأْنَـٰهُنَّ إِنشَآءً﴿٣٥﴾
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
—فَجَعَلْنَـٰهُنَّ أَبْكَارًا﴿٣٦﴾
Na tutawafanya vijana,
—عُرُبًا أَتْرَابًا﴿٣٧﴾
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
—لِّأَصْحَـٰبِ ٱلْيَمِينِ﴿٣٨﴾
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
—ثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ﴿٣٩﴾
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
—وَثُلَّةٌ مِّنَ ٱلْـَٔاخِرِينَ﴿٤٠﴾
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
—وَأَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصْحَـٰبُ ٱلشِّمَالِ﴿٤١﴾
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
—فِى سَمُومٍ وَحَمِيمٍ﴿٤٢﴾
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
—وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ﴿٤٣﴾
Na kivuli cha moshi mweusi,
—لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ﴿٤٤﴾
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
—إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ﴿٤٥﴾
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
—وَكَانُوا۟ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلْحِنثِ ٱلْعَظِيمِ﴿٤٦﴾
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
—وَكَانُوا۟ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَـٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ﴿٤٧﴾
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
—أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ﴿٤٨﴾
Au baba zetu wa zamani?
—قُلْ إِنَّ ٱلْأَوَّلِينَ وَٱلْـَٔاخِرِينَ﴿٤٩﴾
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
—لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَـٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ﴿٥٠﴾
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
—