Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/44

المعارج

Al-Ma'arij

Meâric

Makkiyya·Aya 44

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

70:1
Juz 29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ﴿١﴾

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,

—
70:2
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

لِّلْكَـٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌ﴿٢﴾

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -

—
70:3
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ﴿٣﴾

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

—
70:4
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

تَعْرُجُ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ﴿٤﴾

Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!

—
70:5
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

فَٱصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا﴿٥﴾

Basi subiri kwa subira njema.

—
70:6
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًا﴿٦﴾

Hakika wao wanaiona iko mbali,

—
70:7
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَنَرَىٰهُ قَرِيبًا﴿٧﴾

Na Sisi tunaiona iko karibu.

—
70:8
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ﴿٨﴾

Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.

—
70:9
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ﴿٩﴾

Na milima itakuwa kama sufi.

—
70:10
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا﴿١٠﴾

Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

—
70:11
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ﴿١١﴾

Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,

—
70:12
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَصَـٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ﴿١٢﴾

Na mkewe, na nduguye,

—
70:13
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ﴿١٣﴾

Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,

—
70:14
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ﴿١٤﴾

Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

—
70:15
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

كَلَّآ ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ﴿١٥﴾

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

—
70:16
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ﴿١٦﴾

Unao babua ngozi ya kichwa!

—
70:17
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ﴿١٧﴾

Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.

—
70:18
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ﴿١٨﴾

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

—
70:19
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

۞ إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا﴿١٩﴾

Hakika mtu ameumbwa na papara.

—
70:20
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًا﴿٢٠﴾

Inapo mgusa shari hupapatika.

—
70:21
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا﴿٢١﴾

Na inapo mgusa kheri huizuilia.

—
70:22
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ﴿٢٢﴾

Isipo kuwa wanao sali,

—
70:23
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ﴿٢٣﴾

Ambao wanadumisha Sala zao,

—
70:24
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ﴿٢٤﴾

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

—
70:25
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ﴿٢٥﴾

Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;

—
70:26
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ﴿٢٦﴾

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

—
70:27
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ﴿٢٧﴾

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

—
70:28
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ﴿٢٨﴾

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.

—
70:29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَـٰفِظُونَ﴿٢٩﴾

Na ambao wanahifadhi tupu zao.

—
70:30
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَـٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ﴿٣٠﴾

Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -

—
70:31
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ﴿٣١﴾

Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.

—
70:32
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَـٰنَـٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ﴿٣٢﴾

Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

—
70:33
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَـٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ﴿٣٣﴾

Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

—
70:34
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ﴿٣٤﴾

Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

—
70:35
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

أُو۟لَـٰٓئِكَ فِى جَنَّـٰتٍ مُّكْرَمُونَ﴿٣٥﴾

Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.

—
70:36
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ﴿٣٦﴾

Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?

—
70:37
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ﴿٣٧﴾

Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

—
70:38
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ﴿٣٨﴾

Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?

—
70:39
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

كَلَّآ ۖ إِنَّا خَلَقْنَـٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ﴿٣٩﴾

La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.

—
70:40
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 569

فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَـٰرِقِ وَٱلْمَغَـٰرِبِ إِنَّا لَقَـٰدِرُونَ﴿٤٠﴾

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza

—
70:41
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ﴿٤١﴾

Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

—
70:42
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَـٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ﴿٤٢﴾

Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,

—
70:43
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ﴿٤٣﴾

Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,

—
70:44
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

خَـٰشِعَةً أَبْصَـٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ﴿٤٤﴾

Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.

—
Aya IliyotanguliaAl-HaqqahAya InayofuataNuh