69:36Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
69:37Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
69:38Basi naapa kwa mnavyo viona,
69:39Na msivyo viona,
69:40Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
69:41Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
69:42Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
69:43Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
69:44Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
69:45Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
69:46Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
69:47Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
69:48Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
69:49Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
69:50Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
69:51Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
69:52Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
70:1Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
70:2Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
70:3Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
70:4Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
70:5Basi subiri kwa subira njema.
70:6Hakika wao wanaiona iko mbali,
70:7Na Sisi tunaiona iko karibu.
70:8Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
70:9Na milima itakuwa kama sufi.
70:10Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.