15:91Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
15:92Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
15:93Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
15:94Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
15:95Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
15:96Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
15:97Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
15:98Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
15:99Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
16:1Amri ya Mwenyezi Mungu itafika tu. Basi msiihimize. Ametakasika na Ametukuka na wanayo mshirikisha nayo.
16:2Huwateremsha Malaika na Roho kwa amri yake juu ya amtakaye katika waja wake ili nyinyi muonye kwamba hapana mungu ila Mimi, basi nicheni Mimi.
16:3Ameziumba mbingu na ardhi kwa Haki. Ametukuka na wanayo shirikisha.
16:4Amemuumba mtu kwa tone la manii. Naye mara amekuwa mshindani dhaahiri.
16:5Na nyama hoa amekuumbieni. Katika hao mna vifaa vya kutia joto, na manufaa mengineyo, na baadhi yao mnawala.
16:6Na wanakupeni furaha pale mnapo warudisha jioni na mnapo wapeleka malishoni asubuhi.