19:96Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi.
19:97Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur'ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wachamngu, na uwaonye kwayo watu wabishi.
19:98Na kaumu ngapi tumezihiliki kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?
20:1T'AHA!
20:2Hatukukuteremshia Qur'ani ili upate mashaka.
20:3Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.
20:4Materemsho yatokayo kwa aliye umba ardhi na mbingu zilizo juu.
20:5Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi.
20:6Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi.
20:7Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na duni kuliko siri.
20:8Mwenyezi Mungu! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa.
20:9Na je! Imekufikia hadithi ya Musa?
20:10Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto.
20:11Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Musa!
20:12Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.