50:36Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
50:37Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
50:38Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
50:39Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
50:40Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
50:41Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
50:42Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
50:43Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
50:44Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
50:45Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.
51:1Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
51:2Na zinazo beba mizigo,
51:3Na zinazo kwenda kwa wepesi.
51:4Na zinazo gawanya kwa amri,
51:5Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
51:6Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.