51:52Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
51:53Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
51:54Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
51:55Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
51:56Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
51:57Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
51:58Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
51:59Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
51:60Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
52:1Naapa kwa mlima wa T'ur,
52:2Na Kitabu kilicho andikwa
52:3Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
52:4Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
52:5Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
52:6Na kwa bahari iliyo jazwa,
52:7Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
52:8Hapana wa kuizuia.
52:9Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
52:10Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
52:11Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
52:12Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
52:13Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
52:14(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!