54:50Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
54:51Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
54:52Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
54:53Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
54:54Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
54:55Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
55:1Arrah'man, Mwingi wa Rehema
55:2Amefundisha Qur'ani.
55:3Amemuumba mwanaadamu,
55:4Akamfundisha kubaini.
55:5Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
55:6Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
55:7Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
55:8Ili msidhulumu katika mizani.
55:9Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
55:10Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
55:11Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
55:12Na nafaka zenye makapi, na rehani.
55:13Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
55:14Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
55:15Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
55:16Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
55:17Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
55:18Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?