Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/78

الرحمن

Ar-Rahman

Rahmân

Madaniyya·Aya 78

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

55:1
Juz 27
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

ٱلرَّحْمَـٰنُ﴿١﴾

Arrah'man, Mwingi wa Rehema

—
55:2
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

عَلَّمَ ٱلْقُرْءَانَ﴿٢﴾

Amefundisha Qur'ani.

—
55:3
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ﴿٣﴾

Amemuumba mwanaadamu,

—
55:4
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

عَلَّمَهُ ٱلْبَيَانَ﴿٤﴾

Akamfundisha kubaini.

—
55:5
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

ٱلشَّمْسُ وَٱلْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ﴿٥﴾

Jua na mwezi huenda kwa hisabu.

—
55:6
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

وَٱلنَّجْمُ وَٱلشَّجَرُ يَسْجُدَانِ﴿٦﴾

Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.

—
55:7
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلْمِيزَانَ﴿٧﴾

Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,

—
55:8
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

أَلَّا تَطْغَوْا۟ فِى ٱلْمِيزَانِ﴿٨﴾

Ili msidhulumu katika mizani.

—
55:9
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

وَأَقِيمُوا۟ ٱلْوَزْنَ بِٱلْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا۟ ٱلْمِيزَانَ﴿٩﴾

Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.

—
55:10
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

وَٱلْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ﴿١٠﴾

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.

—
55:11
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

فِيهَا فَـٰكِهَةٌ وَٱلنَّخْلُ ذَاتُ ٱلْأَكْمَامِ﴿١١﴾

Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.

—
55:12
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

وَٱلْحَبُّ ذُو ٱلْعَصْفِ وَٱلرَّيْحَانُ﴿١٢﴾

Na nafaka zenye makapi, na rehani.

—
55:13
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿١٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

—
55:14
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

خَلَقَ ٱلْإِنسَـٰنَ مِن صَلْصَـٰلٍ كَٱلْفَخَّارِ﴿١٤﴾

Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..

—
55:15
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

وَخَلَقَ ٱلْجَآنَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ﴿١٥﴾

Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.

—
55:16
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿١٦﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

—
55:17
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

رَبُّ ٱلْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ ٱلْمَغْرِبَيْنِ﴿١٧﴾

Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.

—
55:18
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 531

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿١٨﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:19
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

مَرَجَ ٱلْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ﴿١٩﴾

Anaziendesha bahari mbili zikutane;

—
55:20
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ﴿٢٠﴾

Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.

—
55:21
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٢١﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:22
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

يَخْرُجُ مِنْهُمَا ٱللُّؤْلُؤُ وَٱلْمَرْجَانُ﴿٢٢﴾

Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.

—
55:23
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٢٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:24
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

وَلَهُ ٱلْجَوَارِ ٱلْمُنشَـَٔاتُ فِى ٱلْبَحْرِ كَٱلْأَعْلَـٰمِ﴿٢٤﴾

Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.

—
55:25
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٢٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:26
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ﴿٢٦﴾

Kila kilioko juu yake kitatoweka.

—
55:27
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو ٱلْجَلَـٰلِ وَٱلْإِكْرَامِ﴿٢٧﴾

Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

—
55:28
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٢٨﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:29
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

يَسْـَٔلُهُۥ مَن فِى ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِى شَأْنٍ﴿٢٩﴾

Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.

—
55:30
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٣٠﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:31
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ ٱلثَّقَلَانِ﴿٣١﴾

Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.

—
55:32
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٣٢﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:33
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

يَـٰمَعْشَرَ ٱلْجِنِّ وَٱلْإِنسِ إِنِ ٱسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا۟ مِنْ أَقْطَارِ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ فَٱنفُذُوا۟ ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَـٰنٍ﴿٣٣﴾

Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.

—
55:34
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٣٤﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:35
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ﴿٣٥﴾

Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.

—
55:36
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٣٦﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:37
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَإِذَا ٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَٱلدِّهَانِ﴿٣٧﴾

Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.

—
55:38
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٣٨﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:39
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٌ وَلَا جَآنٌّ﴿٣٩﴾

Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.

—
55:40
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٤٠﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:41
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 532

يُعْرَفُ ٱلْمُجْرِمُونَ بِسِيمَـٰهُمْ فَيُؤْخَذُ بِٱلنَّوَٰصِى وَٱلْأَقْدَامِ﴿٤١﴾

Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.

—
55:42
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٤٢﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:43
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

هَـٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِى يُكَذِّبُ بِهَا ٱلْمُجْرِمُونَ﴿٤٣﴾

Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.

—
55:44
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ ءَانٍ﴿٤٤﴾

Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.

—
55:45
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٤٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:46
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ﴿٤٦﴾

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.

—
55:47
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٤٧﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:48
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

ذَوَاتَآ أَفْنَانٍ﴿٤٨﴾

Bustani zenye matawi yaliyo tanda.

—
55:49
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

فَبِأَىِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ﴿٤٩﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

—
55:50
Juz 27 · Hizb 54 · Ukurasa 533

فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ﴿٥٠﴾

Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.

—
Aya IliyotanguliaAl-QamarAya InayofuataAl-Waqi'ah