56:77Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
56:78Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
56:79Hapana akigusaye ila walio takaswa.
56:80Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
56:81Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
56:82Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
56:83Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
56:84Na nyinyi wakati huo mnatazama!
56:85Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
56:86Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
56:87Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
56:88Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
56:89Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
56:90Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
56:91Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
56:92Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
56:93Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
56:94Na kutiwa Motoni.
56:95Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
56:96Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
57:1Kinamsabihi kumtakasa Mwenyezi Mungu kila kiliomo ndani ya mbingu na ardhi. Na Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
57:2Yeye ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Anahuisha na anafisha. Na Yeye ni Mwenye uweza wa kila kitu.
57:3Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa Mwisho, naye ndiye wa Dhaahiri na wa Siri, naye ndiye Mjuzi wa kila kitu.