Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/52

الحاقة

Al-Haqqah

Hâkka

Makkiyya·Aya 52

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

69:1
Juz 29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

ٱلْحَآقَّةُ﴿١﴾

Tukio la haki.

—
69:2
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

مَا ٱلْحَآقَّةُ﴿٢﴾

Nini hilo Tukio la haki?

—
69:3
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحَآقَّةُ﴿٣﴾

Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?

—
69:4
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

كَذَّبَتْ ثَمُودُ وَعَادٌۢ بِٱلْقَارِعَةِ﴿٤﴾

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.

—
69:5
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهْلِكُوا۟ بِٱلطَّاغِيَةِ﴿٥﴾

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

—
69:6
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

وَأَمَّا عَادٌ فَأُهْلِكُوا۟ بِرِيحٍ صَرْصَرٍ عَاتِيَةٍ﴿٦﴾

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.

—
69:7
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

سَخَّرَهَا عَلَيْهِمْ سَبْعَ لَيَالٍ وَثَمَـٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومًا فَتَرَى ٱلْقَوْمَ فِيهَا صَرْعَىٰ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ خَاوِيَةٍ﴿٧﴾

Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.

—
69:8
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 566

فَهَلْ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٍ﴿٨﴾

Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?

—
69:9
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَجَآءَ فِرْعَوْنُ وَمَن قَبْلَهُۥ وَٱلْمُؤْتَفِكَـٰتُ بِٱلْخَاطِئَةِ﴿٩﴾

Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.

—
69:10
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فَعَصَوْا۟ رَسُولَ رَبِّهِمْ فَأَخَذَهُمْ أَخْذَةً رَّابِيَةً﴿١٠﴾

Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.

—
69:11
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلْمَآءُ حَمَلْنَـٰكُمْ فِى ٱلْجَارِيَةِ﴿١١﴾

Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,

—
69:12
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

لِنَجْعَلَهَا لَكُمْ تَذْكِرَةً وَتَعِيَهَآ أُذُنٌ وَٰعِيَةٌ﴿١٢﴾

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.

—
69:13
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فَإِذَا نُفِخَ فِى ٱلصُّورِ نَفْخَةٌ وَٰحِدَةٌ﴿١٣﴾

Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,

—
69:14
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَحُمِلَتِ ٱلْأَرْضُ وَٱلْجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةً وَٰحِدَةً﴿١٤﴾

Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,

—
69:15
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فَيَوْمَئِذٍ وَقَعَتِ ٱلْوَاقِعَةُ﴿١٥﴾

Siku hiyo ndio Tukio litatukia.

—
69:16
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِىَ يَوْمَئِذٍ وَاهِيَةٌ﴿١٦﴾

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

—
69:17
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَٱلْمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرْجَآئِهَا ۚ وَيَحْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذٍ ثَمَـٰنِيَةٌ﴿١٧﴾

Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

—
69:18
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

يَوْمَئِذٍ تُعْرَضُونَ لَا تَخْفَىٰ مِنكُمْ خَافِيَةٌ﴿١٨﴾

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

—
69:19
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَـٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقْرَءُوا۟ كِتَـٰبِيَهْ﴿١٩﴾

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

—
69:20
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

إِنِّى ظَنَنتُ أَنِّى مُلَـٰقٍ حِسَابِيَهْ﴿٢٠﴾

Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

—
69:21
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فَهُوَ فِى عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ﴿٢١﴾

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,

—
69:22
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍ﴿٢٢﴾

Katika Bustani ya juu,

—
69:23
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ﴿٢٣﴾

Matunda yake yakaribu.

—
69:24
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَآ أَسْلَفْتُمْ فِى ٱلْأَيَّامِ ٱلْخَالِيَةِ﴿٢٤﴾

Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.

—
69:25
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَـٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَـٰلَيْتَنِى لَمْ أُوتَ كِتَـٰبِيَهْ﴿٢٥﴾

Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!

—
69:26
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ﴿٢٦﴾

Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.

—
69:27
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

يَـٰلَيْتَهَا كَانَتِ ٱلْقَاضِيَةَ﴿٢٧﴾

Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.

—
69:28
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

مَآ أَغْنَىٰ عَنِّى مَالِيَهْ ۜ﴿٢٨﴾

Mali yangu hayakunifaa kitu.

—
69:29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

هَلَكَ عَنِّى سُلْطَـٰنِيَهْ﴿٢٩﴾

Madaraka yangu yamenipotea.

—
69:30
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

خُذُوهُ فَغُلُّوهُ﴿٣٠﴾

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

—
69:31
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

ثُمَّ ٱلْجَحِيمَ صَلُّوهُ﴿٣١﴾

Kisha mtupeni Motoni!

—
69:32
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

ثُمَّ فِى سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَٱسْلُكُوهُ﴿٣٢﴾

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!

—
69:33
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِٱللَّهِ ٱلْعَظِيمِ﴿٣٣﴾

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,

—
69:34
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ﴿٣٤﴾

Wala hahimizi kulisha masikini.

—
69:35
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 567

فَلَيْسَ لَهُ ٱلْيَوْمَ هَـٰهُنَا حَمِيمٌ﴿٣٥﴾

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,

—
69:36
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنْ غِسْلِينٍ﴿٣٦﴾

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

—
69:37
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

لَّا يَأْكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلْخَـٰطِـُٔونَ﴿٣٧﴾

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

—
69:38
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

فَلَآ أُقْسِمُ بِمَا تُبْصِرُونَ﴿٣٨﴾

Basi naapa kwa mnavyo viona,

—
69:39
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَمَا لَا تُبْصِرُونَ﴿٣٩﴾

Na msivyo viona,

—
69:40
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ﴿٤٠﴾

Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.

—
69:41
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِرٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تُؤْمِنُونَ﴿٤١﴾

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.

—
69:42
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَلَا بِقَوْلِ كَاهِنٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ﴿٤٢﴾

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.

—
69:43
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ ٱلْعَـٰلَمِينَ﴿٤٣﴾

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

—
69:44
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَلَوْ تَقَوَّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ ٱلْأَقَاوِيلِ﴿٤٤﴾

Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,

—
69:45
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

لَأَخَذْنَا مِنْهُ بِٱلْيَمِينِ﴿٤٥﴾

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,

—
69:46
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

ثُمَّ لَقَطَعْنَا مِنْهُ ٱلْوَتِينَ﴿٤٦﴾

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!

—
69:47
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

فَمَا مِنكُم مِّنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَـٰجِزِينَ﴿٤٧﴾

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.

—
69:48
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَإِنَّهُۥ لَتَذْكِرَةٌ لِّلْمُتَّقِينَ﴿٤٨﴾

Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.

—
69:49
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَإِنَّا لَنَعْلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ﴿٤٩﴾

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.

—
69:50
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 568

وَإِنَّهُۥ لَحَسْرَةٌ عَلَى ٱلْكَـٰفِرِينَ﴿٥٠﴾

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.

—
Aya IliyotanguliaAl-QalamAya InayofuataAl-Ma'arij