70:41Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
70:42Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
70:43Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
70:44Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
71:1Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
71:2Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
71:3Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
71:4Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
71:5Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
71:6Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
71:7Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
71:8Tena niliwaita kwa uwazi,
71:9Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
71:10Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.