Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/28

نوح

Nuh

Nûh

Makkiyya·Aya 28

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

71:1
Juz 29
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

إِنَّآ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِۦٓ أَنْ أَنذِرْ قَوْمَكَ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿١﴾

Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.

—
71:2
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

قَالَ يَـٰقَوْمِ إِنِّى لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌ﴿٢﴾

Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,

—
71:3
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

أَنِ ٱعْبُدُوا۟ ٱللَّهَ وَٱتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ﴿٣﴾

Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.

—
71:4
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰٓ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ ٱللَّهِ إِذَا جَآءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿٤﴾

Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!

—
71:5
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

قَالَ رَبِّ إِنِّى دَعَوْتُ قَوْمِى لَيْلًا وَنَهَارًا﴿٥﴾

Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,

—
71:6
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَآءِىٓ إِلَّا فِرَارًا﴿٦﴾

Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.

—
71:7
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

وَإِنِّى كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوٓا۟ أَصَـٰبِعَهُمْ فِىٓ ءَاذَانِهِمْ وَٱسْتَغْشَوْا۟ ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا۟ وَٱسْتَكْبَرُوا۟ ٱسْتِكْبَارًا﴿٧﴾

Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!

—
71:8
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

ثُمَّ إِنِّى دَعَوْتُهُمْ جِهَارًا﴿٨﴾

Tena niliwaita kwa uwazi,

—
71:9
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

ثُمَّ إِنِّىٓ أَعْلَنتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًا﴿٩﴾

Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.

—
71:10
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 570

فَقُلْتُ ٱسْتَغْفِرُوا۟ رَبَّكُمْ إِنَّهُۥ كَانَ غَفَّارًا﴿١٠﴾

Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.

—
71:11
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

يُرْسِلِ ٱلسَّمَآءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا﴿١١﴾

Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.

—
71:12
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَٰلٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّـٰتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَـٰرًا﴿١٢﴾

Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.

—
71:13
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

مَّا لَكُمْ لَا تَرْجُونَ لِلَّهِ وَقَارًا﴿١٣﴾

Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?

—
71:14
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَقَدْ خَلَقَكُمْ أَطْوَارًا﴿١٤﴾

Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?

—
71:15
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

أَلَمْ تَرَوْا۟ كَيْفَ خَلَقَ ٱللَّهُ سَبْعَ سَمَـٰوَٰتٍ طِبَاقًا﴿١٥﴾

Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?

—
71:16
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَجَعَلَ ٱلْقَمَرَ فِيهِنَّ نُورًا وَجَعَلَ ٱلشَّمْسَ سِرَاجًا﴿١٦﴾

Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?

—
71:17
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَٱللَّهُ أَنۢبَتَكُم مِّنَ ٱلْأَرْضِ نَبَاتًا﴿١٧﴾

Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.

—
71:18
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

ثُمَّ يُعِيدُكُمْ فِيهَا وَيُخْرِجُكُمْ إِخْرَاجًا﴿١٨﴾

Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.

—
71:19
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ ٱلْأَرْضَ بِسَاطًا﴿١٩﴾

Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.

—
71:20
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

لِّتَسْلُكُوا۟ مِنْهَا سُبُلًا فِجَاجًا﴿٢٠﴾

Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.

—
71:21
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

قَالَ نُوحٌ رَّبِّ إِنَّهُمْ عَصَوْنِى وَٱتَّبَعُوا۟ مَن لَّمْ يَزِدْهُ مَالُهُۥ وَوَلَدُهُۥٓ إِلَّا خَسَارًا﴿٢١﴾

Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.

—
71:22
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَمَكَرُوا۟ مَكْرًا كُبَّارًا﴿٢٢﴾

Na wakapanga vitimbi vikubwa.

—
71:23
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَقَالُوا۟ لَا تَذَرُنَّ ءَالِهَتَكُمْ وَلَا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلَا سُوَاعًا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا﴿٢٣﴾

Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.

—
71:24
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَقَدْ أَضَلُّوا۟ كَثِيرًا ۖ وَلَا تَزِدِ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا ضَلَـٰلًا﴿٢٤﴾

Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.

—
71:25
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

مِّمَّا خَطِيٓـَٔـٰتِهِمْ أُغْرِقُوا۟ فَأُدْخِلُوا۟ نَارًا فَلَمْ يَجِدُوا۟ لَهُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ أَنصَارًا﴿٢٥﴾

Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.

—
71:26
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

وَقَالَ نُوحٌ رَّبِّ لَا تَذَرْ عَلَى ٱلْأَرْضِ مِنَ ٱلْكَـٰفِرِينَ دَيَّارًا﴿٢٦﴾

Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!

—
71:27
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

إِنَّكَ إِن تَذَرْهُمْ يُضِلُّوا۟ عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوٓا۟ إِلَّا فَاجِرًا كَفَّارًا﴿٢٧﴾

Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.

—
71:28
Juz 29 · Hizb 57 · Ukurasa 571

رَّبِّ ٱغْفِرْ لِى وَلِوَٰلِدَىَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِىَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَـٰتِ وَلَا تَزِدِ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا تَبَارًۢا﴿٢٨﴾

Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.

—
Aya IliyotanguliaAl-Ma'arijAya InayofuataAl-Jinn