76:26Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
76:27Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
76:28Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
76:29Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
76:30Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
76:31Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.
77:1Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
77:2Na zinazo vuma kwa kasi!
77:3Na zikaeneza maeneo yote!
77:4Na zinazo farikisha zikatawanya!
77:5Na zinazo peleka mawaidha!
77:6Kwa kuudhuru au kuonya,
77:7Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
77:8Wakati nyota zitakapo futwa,
77:9Na mbingu zitakapo pasuliwa,
77:10Na milima itakapo peperushwa,
77:11Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
77:12Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
77:13Kwa siku ya kupambanua!
77:14Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
77:15Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
77:16Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
77:17Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
77:18Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
77:19Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!