83:34Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
83:35Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
83:36Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
84:1Itapo chanika mbingu,
84:2Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
84:3Na ardhi itakapo tanuliwa,
84:4Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
84:5Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
84:6Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
84:7Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
84:8Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
84:9Na arudi kwa ahali zake na furaha.
84:10Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
84:11Basi huyo ataomba kuteketea.
84:12Na ataingia Motoni.
84:13Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
84:14Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
84:15Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
84:16Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
84:17Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
84:18Na kwa mwezi unapo pevuka,
84:19Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
84:20Basi wana nini hawaamini?
84:21Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
84:22Bali walio kufuru wanakanusha tu.
84:23Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
84:24Basi wabashirie adhabu chungu!