84:25Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
85:1Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
85:2Na kwa siku iliyo ahidiwa!
85:3Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
85:4Wameangamizwa watu wa makhandaki
85:5Yenye moto wenye kuni nyingi,
85:6Walipo kuwa wamekaa hapo,
85:7Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
85:8Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
85:9Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
85:10Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
85:11Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
85:12Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
85:13Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
85:14Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
85:15Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
85:16Atendaye ayatakayo.
85:17Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
85:18Ya Firauni na Thamudi?
85:19Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
85:20Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
85:21Bali hii ni Qur'ani tukufu
85:22Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.