Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/22

البروج

Al-Buruj

Bürûc

Makkiyya·Aya 22

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

85:1
Juz 30
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ﴿١﴾

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

—
85:2
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ﴿٢﴾

Na kwa siku iliyo ahidiwa!

—
85:3
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ﴿٣﴾

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

—
85:4
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

قُتِلَ أَصْحَـٰبُ ٱلْأُخْدُودِ﴿٤﴾

Wameangamizwa watu wa makhandaki

—
85:5
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ﴿٥﴾

Yenye moto wenye kuni nyingi,

—
85:6
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ﴿٦﴾

Walipo kuwa wamekaa hapo,

—
85:7
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ﴿٧﴾

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

—
85:8
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ﴿٨﴾

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

—
85:9
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍ شَهِيدٌ﴿٩﴾

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

—
85:10
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَـٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ﴿١٠﴾

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

—
85:11
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ لَهُمْ جَنَّـٰتٌ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَـٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ﴿١١﴾

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

—
85:12
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ﴿١٢﴾

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

—
85:13
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ﴿١٣﴾

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

—
85:14
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ﴿١٤﴾

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

—
85:15
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ﴿١٥﴾

Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

—
85:16
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ﴿١٦﴾

Atendaye ayatakayo.

—
85:17
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ﴿١٧﴾

Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

—
85:18
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ﴿١٨﴾

Ya Firauni na Thamudi?

—
85:19
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍ﴿١٩﴾

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

—
85:20
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ﴿٢٠﴾

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

—
85:21
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

بَلْ هُوَ قُرْءَانٌ مَّجِيدٌ﴿٢١﴾

Bali hii ni Qur'ani tukufu

—
85:22
Juz 30 · Hizb 59 · Ukurasa 590

فِى لَوْحٍ مَّحْفُوظٍۭ﴿٢٢﴾

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.

—
Aya IliyotanguliaAl-InshiqaqAya InayofuataAt-Tariq