89:23Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
89:24Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
89:25Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
89:26Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
89:27Ewe nafsi iliyo tua!
89:28Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
89:29Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
89:30Na ingia katika Pepo yangu.
90:1Naapa kwa Mji huu!
90:2Nawe unaukaa Mji huu.
90:3Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
90:4Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
90:5Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
90:6Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
90:7Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
90:8Kwani hatukumpa macho mawili?
90:9Na ulimi, na midomo miwili?
90:10Na tukambainishia zote njia mbili?
90:11Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
90:12Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
90:13Kumkomboa mtumwa;
90:14Au kumlisha siku ya njaa
90:15Yatima aliye jamaa,
90:16Au masikini aliye vumbini.
90:17Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
90:18Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.